Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 50:25-30 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Nimefungua ghala yangu ya silaha,nikatoa humo silaha za ghadhabu yangu,maana mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshinina kazi ya kufanyakatika nchi ya Wakaldayo.

26. Njoni mkamshambulie kutoka kila upande;zifungueni ghala zake za chakula;mrundikieni marundo ya nafaka!Iangamizeni kabisa nchi hii;msibakize chochote!

27. Waueni askari wake hodari;waache washukie machinjoni.Ole wao, maana siku yao imewadia,wakati wao wa kuadhibiwa umefika.

28. “Sikiliza! Wakimbizi na watoro kutoka nchi ya Babuloni wanakuja kutangaza huko Siyoni jinsi Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.

29. “Waiteni wapiga mishale waishambulie Babuloni. Pelekeni kila mtu ajuaye kuvuta upinde. Uzingireni mji pasiwe na yeyote atakayetoroka. Ulipizeni kadiri ya matendo yake yote; utendeeni kama ulivyowatendea wengine, maana kwa kiburi ulinidharau mimi Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli.

30. Kwa hiyo, vijana wake watauawa katika mitaa yake, na majeshi yake yote yataangamizwa siku hiyo. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

Kusoma sura kamili Yeremia 50