24. Ewe Babuloni, nilikutegea mtego ukanaswa,wala hukujua juu yake;ulipatikana, ukakamatwa,kwa sababu ulishindana nami Mwenyezi-Mungu.
25. Nimefungua ghala yangu ya silaha,nikatoa humo silaha za ghadhabu yangu,maana mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshinina kazi ya kufanyakatika nchi ya Wakaldayo.
26. Njoni mkamshambulie kutoka kila upande;zifungueni ghala zake za chakula;mrundikieni marundo ya nafaka!Iangamizeni kabisa nchi hii;msibakize chochote!
27. Waueni askari wake hodari;waache washukie machinjoni.Ole wao, maana siku yao imewadia,wakati wao wa kuadhibiwa umefika.