10. Nchi ya Wakaldayo itaporwa, na hao watakaoipora wataridhika. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
11. “Enyi waporaji wa mali yangu!Japo mnafurahi na kushangilia,mnarukaruka kama mtamba wa ng'ombe anayepura nafaka,na kulia kama farasi dume,
12. nchi yenu ya kuzaliwa itaaibishwa;hiyo nchi mama yenu itafedheheshwa.Lo! Babuloni itakuwa ya mwisho kati ya mataifa,itakuwa nyika kame na jangwa.