Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 5:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kimbieni huko na huko mjini Yerusalemu;pelelezeni na kujionea wenyewe!Chunguzeni masoko yakemwone kama kuna mtu atendaye hakimtu atafutaye ukweli;akiwako, basi Mwenyezi-Mungu atausamehe Yerusalemu.

2. Ingawa wanaapa: “Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo”,viapo vyao ni vya uongo.

3. Ee Mwenyezi-Mungu, wewe watafuta daima uaminifu.Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu;umewateketeza, lakini walikataa kukosolewa.Wamezifanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba;wamekataa kabisa kurudi kwako.

Kusoma sura kamili Yeremia 5