Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 49:8-15 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Kimbieni enyi wakazi wa Dedani;geukeni mkaishi mafichoni!Maana nitawaleteeni maangamizienyi wazawa wa Esau;wakati wa kuwaadhibu umefika.

9. Wachuma zabibu watakapokuja kwenuhawatabakiza hata zabibu moja.Usiku ule wezi watakapofika,wataharibu kila kitu mpaka watosheke.

10. Lakini nimemnyanganya Esau kila kitu,naam, nimeyafunua maficho yake,wala hawezi kujificha tena.Watoto, ndugu na jirani zake wameangamizwa;hakuna hata mmoja aliyebaki.

11. Niachieni watoto wenu yatima nami nitawatunza;waacheni wajane wenu wanitegemee.”

12. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Ikiwa wale ambao hawakustahili kunywa kikombe cha adhabu ni lazima wanywe, je, wewe utaachwa bila kuadhibiwa? La! Hutakosa kuadhibiwa; ni lazima unywe hicho kikombe!

13. Maana nimeapa kwa nafsi yangu kwamba mji wa Bosra utakuwa kioja na kichekesho, utakuwa uharibifu na laana; vijiji vyote vitakuwa magofu daima. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

14. Nimepata habari kutoka kwa Mwenyezi-Mungu,mjumbe ametumwa ayatangazie mataifa:“Jikusanyeni pamoja dhidi ya Edomu;inukeni mwende kuushambulia!

15. Mimi Mwenyezi-Mungu nitakufanya wee Edomukuwa mdogo kuliko mataifa yote.Ulimwengu wote utakudharau.

Kusoma sura kamili Yeremia 49