Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 49:15-28 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Mimi Mwenyezi-Mungu nitakufanya wee Edomukuwa mdogo kuliko mataifa yote.Ulimwengu wote utakudharau.

16. Vitisho unavyotoa na kiburi chako vimekudanganya,ewe ukaaye katika mapango ya miamba,unayeishi juu ya kilele cha mlima!Ingawa unaweka makao yako juu kama ya tai,mimi nitakuporomosha kutoka huko uliko.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

17. “Edomu itakuwa kitisho na kila mtu atakayepita karibu yake atashangaa, na kuizomea kwa sababu ya maafa yatakayoipata.

18. Kama vile Sodoma na Gomora na miji jirani yake ilivyoangamizwa, mimi Mwenyezi-Mungu nasema, hakutakuwa na mtu yeyote atakayeishi Edomu wala kufanya mashauri humo.

19. Kama vile simba anavyochomoza kutoka msitu wa mto Yordani na kuingia kwenye malisho mazuri, ndivyo nitakavyowafukuza ghafla Waedomu kutoka nchi yao. Nami nitamweka huko kiongozi yeyote nitakayemchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani awezaye kunishtaki? Ni mchungaji gani awezaye kunipinga?

20. Kwa hiyo, sikilizeni mpango ambao mimi Mwenyezi-Mungu nimepanga dhidi ya Edomu pamoja na mambo niliyokusudia kuwafanyia wakazi wa Temani: Hakika, watoto wao wadogo wataburutwa na kuchukuliwa; kweli kutakuwa na mshangao mkubwa katika makao yao!

21. Kwa kishindo cha kuanguka kwao, dunia itatetemeka; sauti ya kilio chao itasikika mpaka bahari ya Shamu.

22. Tazama, adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosra. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakumbwa na hofu kama ya mwanamke anayejifungua.”

23. Kuhusu Damasko:“Miji ya Hamathi na Arpadi, imejaa wasiwasikwa kufikiwa na habari mbaya;mioyo ya watu wake inayeyuka kwa hofu,imefadhaika kama bahari isiyoweza kutulia.

24. Watu wa Damasko wamekufa moyo;wamegeuka wapate kukimbia;hofu kubwa imewakumba,uchungu na huzuni vimewapata,kama mwanamke anayejifungua

25. Ajabu kuachwa kwa mji maarufu,mji uliokuwa umejaa furaha!

26. Basi vijana wake wataanguka viwanjani mwake,askari wake wote wataangamizwa siku hiyo.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.

27. Nitawasha moto katika kuta za Damasko,nao utateketeza ngome za mfalme Ben-hadadi.”

28. Kuhusu Kedari na falme za Hazori ambazo Nebukadneza mfalme wa Babuloni, alizishambulia na kuzishinda, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Inuka uende kulishambulia kabila la Kedari!Waangamize watu wa mashariki!

Kusoma sura kamili Yeremia 49