Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 48:6-16 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Kimbieni! Jiokoeni wenyewe!Kimbieni kama pundamwitu jangwani!

7. “Moabu, ulitumainia ngome na hazina zako,lakini sasa wewe pia utatekwa;mungu wako Kemoshi atapelekwa uhamishonipamoja na makuhani na watumishi wake.

8. Mwangamizi atapita katika kila mji,hakuna mji utakaomwepa;kila kitu mabondeni kitaangamianyanda za juu zitaharibiwa,kama alivyosema Mwenyezi-Mungu.

9. Mchimbieni Moabu kaburi,maana kuangamia kwake ni hakika;miji yake itakuwa tupu,bila mkazi hata mmoja.

10. Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Mwenyezi-Mungu kwa ulegevu; alaaniwe anayezuia upanga wake usimwage damu!

11. Moabu amestarehe tangu ujana wake,ametulia kama divai katika gudulia.Hajamiminiwa toka chombo hata chombo,hajapata kuchukuliwa uhamishoni.Kwa hiyo yungali na ladha yake,harufu yake nzuri haijabadilika kamwe.

12. “Kwa hiyo, wakati waja, nasema mimi Mwenyezi-Mungu ambapo nitampelekea wamiminaji ambao wataimimina divai yake. Wataimwaga yote kutoka vyombo vyake na kuvivunja vipandevipande.

13. Hapo Wamoabu watamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile watu wa Israeli walivyomwonea aibu Betheli, mungu waliyemtegemea.

14. Mwawezaje kusema: ‘Sisi ni mashujaa,na watu wenye nguvu nyingi za vita?’

15. Mwangamizi wa Moabu na miji yake amewasilivijana wake wazuri wamechinjwa.Nimesema mimi mfalmeniitwaye Mwenyezi-Mungu wa Majeshi.

16. Janga la Moabu limekaribia,maangamizi yake yanawasili haraka.

Kusoma sura kamili Yeremia 48