Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 48:29-33 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu;Moabu ana majivuno sana.Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake;tumesikia jinsi anavyojigamba moyoni.

30. “Nami Mwenyezi-Mungu nasema:Najua ufidhuli wake;Majivuno yake ni ya bure,na matendo yake si kitu.

31. Kwa hiyo ninaomboleza juu ya Moabu,ninalia kwa ajili ya Wamoabu wote,naomboleza juu ya watu wa Kir-heresi.

32. Nakulilia wewe bustani ya Sibmakuliko hata watu wa Yazeri.Matawi yako yametandampaka ngambo ya bahari ya Chumviyakafika hata mpaka Yazeri.Lakini mwangamizi ameyakumbamatunda yako ya kiangazi na zabibu zako.

33. Furaha na shangwe zimeondolewakutoka nchi ya Moabu yenye rutuba.Nimeikomesha divai kutoka mashinikizohakuna mtu anayekamua zabibu kwa shangwe;kelele zinazosikika si za shangwe.

Kusoma sura kamili Yeremia 48