Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 48:24-36 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Keriothi na Bosra. Naam, hukumu imeifikia miji yote ya Moabu mbali na karibu.

25. Nguvu za Moabu zimevunjiliwa mbali na uwezo wake umevunjwa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

26. “Mlewesheni Moabu kwa sababu alijikuza dhidi yangu mimi Mwenyezi-Mungu. Moabu atagaagaa katika matapishi yake na watu watamcheka.

27. Kumbuka Moabu ulivyomcheka Israeli. Je, alikamatwa pamoja na wezi, hata ukawa unatikisa kichwa chako kila ulipoongea juu yake?

28. “Enyi wenyeji wa Moabu,tokeni mijini, mkakae mapangoni!Mwigeni njiwa ajengaye kiota penye genge.

29. Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu;Moabu ana majivuno sana.Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake;tumesikia jinsi anavyojigamba moyoni.

30. “Nami Mwenyezi-Mungu nasema:Najua ufidhuli wake;Majivuno yake ni ya bure,na matendo yake si kitu.

31. Kwa hiyo ninaomboleza juu ya Moabu,ninalia kwa ajili ya Wamoabu wote,naomboleza juu ya watu wa Kir-heresi.

32. Nakulilia wewe bustani ya Sibmakuliko hata watu wa Yazeri.Matawi yako yametandampaka ngambo ya bahari ya Chumviyakafika hata mpaka Yazeri.Lakini mwangamizi ameyakumbamatunda yako ya kiangazi na zabibu zako.

33. Furaha na shangwe zimeondolewakutoka nchi ya Moabu yenye rutuba.Nimeikomesha divai kutoka mashinikizohakuna mtu anayekamua zabibu kwa shangwe;kelele zinazosikika si za shangwe.

34. “Kilio cha watu wa Heshboni chasikika huko Eleale mpaka Yahazi; kinaenea kutoka Soari mpaka Horonaimu na hata Eglath-shelishiya. Hata maji ya kijito Nimrimu yamekauka.

35. Nami nitamfutilia mbali kila mtu katika Moabu ambaye anatambikia vilimani na kumfukizia ubani mungu wake.

36. “Kwa hiyo, moyo wangu unaomboleza juu ya watu wa Moabu na watu wa Kir-heresi, kama mpiga zumari mazishini; maana hata mali yote waliyojipatia imeangamia.

Kusoma sura kamili Yeremia 48