Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 48:2-9 Biblia Habari Njema (BHN)

2. fahari ya Moabu imetoweka.Mpango ulifanywa huko Heshboni dhidi yake:‘Haya! Tuwaangamize wasiwe tena taifa!’Nawe Madmeni utanyamazishwa,upanga utakufuatia.

3. Sikiliza! Kilio kutoka Horonaimu:‘Maangamizi na uharibifu mkubwa!’

4. Moabu tayari imeangamizwakilio chake chasikika mpaka Soari.

5. Walionusurika wanapanda kwenda Luhithihuku wanalia kwa sauti.Wanapoteremka kwenda Horonaimu,wanasikia kilio cha uharibifu.

6. Kimbieni! Jiokoeni wenyewe!Kimbieni kama pundamwitu jangwani!

7. “Moabu, ulitumainia ngome na hazina zako,lakini sasa wewe pia utatekwa;mungu wako Kemoshi atapelekwa uhamishonipamoja na makuhani na watumishi wake.

8. Mwangamizi atapita katika kila mji,hakuna mji utakaomwepa;kila kitu mabondeni kitaangamianyanda za juu zitaharibiwa,kama alivyosema Mwenyezi-Mungu.

9. Mchimbieni Moabu kaburi,maana kuangamia kwake ni hakika;miji yake itakuwa tupu,bila mkazi hata mmoja.

Kusoma sura kamili Yeremia 48