18. Enyi wenyeji wa Diboni:Shukeni kutoka mahali penu pa fahari,mkaketi katika ardhi isiyo na maji.Maana mwangamizi wa Moabu,amefika kuwashambulia;amekwisha haribu ngome zenu.
19. Enyi wakazi wa Aroeri,simameni kando ya njia mtazame!Mwulizeni anayekimbia na anayetoroka:‘Kumetokea nini?’
20. Moabu imeaibishwa maana imevunjwa;ombolezeni na kulia.Tangazeni kando ya mto Arnoni,kwamba Moabu imeharibiwa kabisa.
21. “Hukumu imeifikia miji iliyo nyanda za juu: Holoni, Yasa, Mefaathi,
22. Diboni, Nebo, Beth-diblathaimu,
23. Kiriathaimu, Beth-gamuli, Beth-meoni,