Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 48:18-23 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Enyi wenyeji wa Diboni:Shukeni kutoka mahali penu pa fahari,mkaketi katika ardhi isiyo na maji.Maana mwangamizi wa Moabu,amefika kuwashambulia;amekwisha haribu ngome zenu.

19. Enyi wakazi wa Aroeri,simameni kando ya njia mtazame!Mwulizeni anayekimbia na anayetoroka:‘Kumetokea nini?’

20. Moabu imeaibishwa maana imevunjwa;ombolezeni na kulia.Tangazeni kando ya mto Arnoni,kwamba Moabu imeharibiwa kabisa.

21. “Hukumu imeifikia miji iliyo nyanda za juu: Holoni, Yasa, Mefaathi,

22. Diboni, Nebo, Beth-diblathaimu,

23. Kiriathaimu, Beth-gamuli, Beth-meoni,

Kusoma sura kamili Yeremia 48