Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 37:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Mfalme Sedekia aliwatuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia, wamwombe awaombee kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.

4. Wakati huo, Yeremia alikuwa bado ana uhuru kutembea miongoni mwa watu, maana alikuwa bado hajatiwa gerezani.

5. Tena jeshi la Farao lilikuwa limeondoka Misri, na jeshi la Wakaldayo lililokuwa limeuzingira mji wa Yerusalemu liliposikia habari hizo liliondoka.

6. Ndipo neno la Mwenyezi-Mungu likamjia nabii Yeremia:

Kusoma sura kamili Yeremia 37