Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 31:27-31 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Mwenyezi-Mungu asema: “Tazama, siku zaja ambapo nitaijaza nchi ya Israeli na nchi ya Yuda watu na wanyama kama mkulima asiavyo mbegu.

28. Na kadiri nilivyokuwa mwangalifu kuwangoa, kuwabomoa, kuwaangusha, kuwaharibu na kuwatesa, ndivyo nitakavyokuwa mwangalifu kuwapanda na kuwajenga.

29. Siku hizo watu hawatasema tena:‘Wazee walikula zabibu chungu,na meno ya watoto yakatiwa ganzi.’

30. La! Kila mmoja atakufa kwa sababu ya dhambi zake mwenyewe; ni yule tu atakayekula zabibu mbivu ndiye meno yake yatatiwa ganzi.”

31. Mwenyezi-Mungu asema: “Siku zaja ambapo nitafanya agano jipya na watu wa Israeli na watu wa Yuda.

Kusoma sura kamili Yeremia 31