Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 31:22-30 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Utasitasita mpaka liniewe binti usiye mwaminifu?Maana, mimi nimefanya kitu kipya duniani:Mwanamke amtafuta mwanamume.”

23. Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: “Nitakapowafanikisha tena watu wa Israeli, wao watatangaza tena katika nchi ya Yuda na katika miji yake wakisema:‘Mwenyezi-Mungu akubariki ewe makao adili,akubariki ee mlima mtakatifu!’

24. “Ndipo watu wa Yuda na miji yake yote, wakulima na wachungaji wanaopitapita na makundi yao, watakaa huko pamoja.

25. Waliochoka nitawachangamsha, na walegevu nitawapa nguvu.

26. Ndio maana mtu ataweza kusema: ‘Niliamka nikatambua kwamba usingizi wangu ulinifaa sana.’”

27. Mwenyezi-Mungu asema: “Tazama, siku zaja ambapo nitaijaza nchi ya Israeli na nchi ya Yuda watu na wanyama kama mkulima asiavyo mbegu.

28. Na kadiri nilivyokuwa mwangalifu kuwangoa, kuwabomoa, kuwaangusha, kuwaharibu na kuwatesa, ndivyo nitakavyokuwa mwangalifu kuwapanda na kuwajenga.

29. Siku hizo watu hawatasema tena:‘Wazee walikula zabibu chungu,na meno ya watoto yakatiwa ganzi.’

30. La! Kila mmoja atakufa kwa sababu ya dhambi zake mwenyewe; ni yule tu atakayekula zabibu mbivu ndiye meno yake yatatiwa ganzi.”

Kusoma sura kamili Yeremia 31