Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 3:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Mume akimpa talaka mkewe,naye akaondoka kwake,na kuwa mke wa mwanamume mwingine,je mume yule aweza kumrudia mwanamke huyo?Je, kufanya hivyo hakutaitia nchi unajisi mkubwa?Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi,je, sasa unataka kunirudia mimi?

2. Inua macho uvitazame vilele vya vilima!Pako wapi mahali ambapo hawajalala nawe?Uliwangoja wapenzi wako kando ya njia,kama bedui aviziavyo watu jangwani.Umeifanya nchi kuwa najisi,kwa ukahaba wako mbaya kupindukia.

3. Ndiyo maana manyunyu yamezuiliwa,na wala mvua za vuli hazijanyesha.Hata hivyo uko macho makavu kama kahaba,huna haya hata kidogo.

Kusoma sura kamili Yeremia 3