23. wakazi wa Dedani, Tema, Buzi na watu wote wanyoao denge;
24. wafalme wote wa Arabia; wafalme wote wa makabila yaliyochanganyika jangwani;
25. wafalme wote wa Zimri, Elamu na Media;
26. wafalme wote wa kaskazini, mbali na karibu, mmoja baada ya mwingine. Falme zote ulimwenguni zitakunywa. Na, baada ya hao wote naye mfalme wa Babuloni atakunywa.
27. Mwenyezi-Mungu akaniamuru: “Utawaambia kuwa mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, nasema hivi: Kunyweni, mlewe na kutapika; angukeni wala msiinuke tena, kwa sababu ya mauaji ninayosababisha miongoni mwenu.
28. Kama wakikataa kukipokea kikombe hicho mkononi mwako na kunywa, wewe utawaambia kuwa mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, nasema kwamba ni lazima wanywe!
29. Tazama! Sasa ninaanza kuleta maafa katika mji unaoitwa kwa jina langu; je, mnadhani mnaweza kuepukana na adhabu? Hamtaachwa bila kuadhibiwa, maana ninaleta mauaji dhidi ya wakazi wote wa dunia. Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.
30. “Basi, wewe Yeremia utatabiri maneno haya yote dhidi yao, na kusema hivi:Mwenyezi-Mungu atanguruma kutoka juu,atatoa sauti yake kutoka makao yake matakatifu;atanguruma kwa nguvu dhidi ya watu wake,na kupaza sauti kama wenye kusindika zabibu,dhidi ya wakazi wote wa dunia.
31. Vishindo hivyo vitasikika hadi mwisho wa dunia,maana Mwenyezi-Mungu ana mashtaka dhidi ya mataifa;anawahukumu wanadamu wote,na waovu atawaua kwa upanga!Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
32. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema:“Tazama, maafa yatalikumba taifa moja baada ya lingine,na tufani itazuka kutoka miisho ya dunia.”
33. Siku hiyo, watakaouawa na Mwenyezi-Mungu watatapakaa kutoka upande mmoja wa dunia hadi mwingine. Hawataombolezewa, hawatakusanywa wala kuzikwa; watabaki kuwa mavi juu ya ardhi.