Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 25:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Basi, nikachukua hicho kikombe mkononi mwa Mwenyezi-Mungu, nikayanywesha mataifa yote ambayo Mwenyezi-Mungu alinituma kwao.

18. Kwanza Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na viongozi wake, ili kuifanya iwe jangwa, ukiwa, kitu cha kuzomewa na kulaaniwa, kama ilivyo mpaka leo. Halafu:

19. Farao, mfalme wa Misri, maofisa na viongozi wake, pamoja na watu wake wote;

20. wageni wote walioishi nchini Misri; wafalme wote wa nchi ya Uzi; wafalme wote wa miji ya Wafilisti, Ashkeloni, Gaza, Ekroni na mabaki ya Ashdodi.

Kusoma sura kamili Yeremia 25