Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 20:10-17 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Nasikia wengi wakinongona juu yangu.Wananipanga jina: “Kitisho kila upande!”Wengine wanasema:“Nendeni mkamshtaki! Na tumshtaki!”Hata rafiki zangu wote wapenzi wanangojea tu nianguke!Wanasema “Labda atadanganyika, nasi tutalipiza kisasi.”

11. Lakini wewe Mwenyezi-Mungu u pamoja namikwangu wewe ni kama shujaa wa kutisha;kwa hiyo watesi wangu watajikwaa,na hawataweza kunishinda.Wataaibika kupindukia,maana hawatafaulu.Fedheha yao itakuwa ya daima;kamwe haitasahaulika.

12. Ee Mwenyezi-Mungu wa majeshi,wewe humthibiti mtu mwadilifu,huona yaliyo moyoni na akilini mwa watu,unijalie kuona ukiwalipiza kisasi,maana kwako nimekiweka kisa changu.

13. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu;msifuni Mwenyezi-Mungu,kwani ameyaokoa maisha ya mhitaji,kutoka mikononi mwa watu waovu.

14. Na ilaaniwe siku niliyozaliwa!Siku hiyo mama aliponizaa,isitakiwe baraka!

15. Na alaaniwe aliyempelekea baba ujumbe:“Umepata mtoto wa kiume”,akamfanya ajae furaha.

16. Mtu huyo na awe kama mijialiyoiangusha Mwenyezi-Mungu bila huruma.Mtu huyo na asikie kilio asubuhi,na mchana kelele za vita,

17. kwani hakuniua tumboni mwa mama yangu;mama yangu angekuwa kaburi langu,tumbo lake lingebaki kubwa daima.

Kusoma sura kamili Yeremia 20