Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 2:5-22 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wazee wenu waliona kosa gani kwanguhata wakanigeuka na kuniacha,wakakimbilia miungu duni,hata nao wakawa watu duni?

6. Hawakujiuliza:‘Yuko wapi Mwenyezi-Mungu aliyetutoa nchini Misri,aliyetuongoza nyikanikatika nchi ya jangwa na makorongo,nchi kame na yenye giza nene,nchi isiyopitiwa na mtu yeyote,wala kukaliwa na binadamu?’

7. Niliwaleta katika nchi yenye rutuba,muyafurahie mazao yake na mema yake mengine.Lakini mlipofika tu mliichafua nchi yangu,mkaifanya chukizo nchi niliyowapa iwe yenu.

8. Nao makuhani hawakujiuliza: ‘Yuko wapi Mwenyezi-Mungu?’Wataalamu wa sheria hawakunijua,viongozi wa watu waliniasi;manabii nao walitabiri kwa jina la Baalina kuabudu sanamu zisizo na faida yoyote.”

9. Mwenyezi-Mungu asema,“Kwa hiyo, mimi nitawalaumu nyinyi,na nitawalaumu wazawa wenu.

10. Haya, vukeni bahari hadi Kupro mkaone,au tumeni watu huko Kedari wakachunguze,kama jambo kama hili limewahi kutokea:

11. Kwamba kuna taifa lililowahi kubadilisha miungu yakeingawa miungu hiyo si miungu!Lakini watu wangu wameniacha mimi, utukufu wao,wakafuata miungu isiyofaa kitu.

12. Shangaeni enyi mbingu, juu ya jambo hili,mkastaajabu na kufadhaika kabisa.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

13. Maana, watu wangu wametenda maovu mawili;wameniacha mimi niliye chemchemi ya maji ya uhai,wakajichimbia visima vyao wenyewe,visima vyenye nyufa, visivyoweza kuhifadhi maji.

14. “Je, Israeli ni mtumwa,ama amezaliwa utumwani?Mbona basi amekuwa kama mawindo?

15. Simba wanamngurumia,wananguruma kwa sauti kubwa.Nchi yake wameifanya jangwa,miji yake imekuwa magofu, haina watu.

16. Isitoshe, watu wa Memfisi na Tahpanesi,wameuvunja utosi wake.

17. Israeli, je, hayo yote si umejiletea mwenyewe,kwa kuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,niliyekuwa ninakuongoza njiani?

18. Na sasa itakufaa nini kwenda Misri,kunywa maji ya mto Nili?Au itakufaa nini kwenda Ashuru,kunywa maji ya mto Eufrate?

19. Uovu wako utakuadhibu;na uasi wako utakuhukumu.Ujue na kutambua kuwa ni vibaya mnokuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,na kuondoa uchaji wangu ndani yako.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.

20. “Tangu zamani wewe ulivunja nira yako,ukaikatilia mbali minyororo yako,ukasema, ‘Sitakutumikia’.Juu ya kila kilima kirefuna chini ya kila mti wa majani mabichi,uliinamia miungu ya rutuba kama kahaba.

21. Lakini mimi nilikupanda kama mzabibu mteule,mzabibu wenye afya na wa mbegu safi;mbona basi umeharibika,ukageuka kuwa mzabibu mwitu?

22. Hata ukijiosha kwa magadi,na kutumia sabuni nyingi,madoa ya uovu wako bado yatabaki mbele yangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

Kusoma sura kamili Yeremia 2