Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 2:16-20 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Isitoshe, watu wa Memfisi na Tahpanesi,wameuvunja utosi wake.

17. Israeli, je, hayo yote si umejiletea mwenyewe,kwa kuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,niliyekuwa ninakuongoza njiani?

18. Na sasa itakufaa nini kwenda Misri,kunywa maji ya mto Nili?Au itakufaa nini kwenda Ashuru,kunywa maji ya mto Eufrate?

19. Uovu wako utakuadhibu;na uasi wako utakuhukumu.Ujue na kutambua kuwa ni vibaya mnokuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,na kuondoa uchaji wangu ndani yako.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.

20. “Tangu zamani wewe ulivunja nira yako,ukaikatilia mbali minyororo yako,ukasema, ‘Sitakutumikia’.Juu ya kila kilima kirefuna chini ya kila mti wa majani mabichi,uliinamia miungu ya rutuba kama kahaba.

Kusoma sura kamili Yeremia 2