Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 15:17-21 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Sikuketi pamoja na wanaostarehe,wala sikufurahi pamoja nao.Niliketi peke yangu nimelemewa nguvu yako;kwa maana ulinijaza hasira yako.

18. Kwa nini mateso yangu hayaishi?Mbona jeraha langu haliponi,wala halitaki kutibiwa?Ama kweli umenidanganya,kama kijito cha maji ya kukaukakauka!”

19. Mwenyezi-Mungu akajibu:“Kama ukinirudia nitakurudishia hali ya kwanza,nawe utanitumikia tena.Kama ukisema maneno ya maana na sio ya upuuzi,basi utakuwa msemaji wangu.Watu watakuja kujumuika nawe,wala sio wewe utakayekwenda kwao.

20. Mbele ya watu hawa,nitakufanya ukuta imara wa shaba.Watapigana nawe,lakini hawataweza kukushinda,maana, mimi niko pamoja nawe,kukuokoa na kukukomboa.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

21. Nitakuokoa mikononi mwa watu waovu,na kukukomboa makuchani mwa wakatili.”

Kusoma sura kamili Yeremia 15