Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 14:6-12 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Pundamwitu wanasimama juu ya vilele vikavu,wanatweta kwa kukosa hewa kama mbweha;macho yao yanafifia kwa kukosa chakula.

7. “Nao watu wanasema:Ingawa dhambi zetu zashuhudia dhidi yetu,utusaidie ee Mwenyezi-Mungu kwa heshima ya jina lako.Maasi yetu ni mengi,tumetenda dhambi dhidi yako.

8. Ewe uliye tumaini la Israeli,mwokozi wetu wakati wa taabu,utakuwaje kama mgeni nchini mwetu,kama msafiri alalaye usiku mmoja?

9. Utakuwaje kama mtu uliyechanganyikiwa,kama shujaa asiyeweza kusaidia mtu?Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu, u pamoja nasi;sisi twaitwa kwa jina lako, usituache.”

10. Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya watu hawa:“Kweli wamependa sana kutangatanga,wala hawakujizuia;kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu siwapokei.Sasa nitayakumbuka makosa yao,na kuwaadhibu kwa dhambi zao.”

11. Mwenyezi-Mungu aliniambia hivi: “Usiwaombee watu hawa fanaka.

12. Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza na za nafaka, mimi sitazikubali. Bali nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”

Kusoma sura kamili Yeremia 14