Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 1:9-13 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Kisha Mwenyezi-Mungu akaunyosha mkono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia,“Tazama nimeyatia maneno yangu kinywani mwako.

10. Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme,uwe na mamlaka ya kungoa na kubomoa,mamlaka ya kuharibu na kuangamiza,mamlaka ya kujenga na ya kupanda.”

11. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: “Yeremia, unaona nini?” Nami nikasema, “Ninaona tawi la mlozi unaochanua.”

12. Mwenyezi-Mungu akaniambia, “Umeona vizuri, maana niko macho kulitekeleza neno langu.”

13. Neno la Mwenyezi-Mungu likanijia mara ya pili: “Unaona nini?” Nami nikasema, “Ninaona chungu kinatokota kimeinama upande wangu kutoka kaskazini.”

Kusoma sura kamili Yeremia 1