Agano la Kale

Agano Jipya

Walawi 21:3-7 Biblia Habari Njema (BHN)

3. au dada yake ambaye (aliye wa jamaa yake ya karibu), naye hajaolewa bado.

4. Yeye, akiwa mwenye madaraka katika jamaa yake, asijitie unajisi.

5. Wazawa wa Aroni kamwe wasijinyoe upara kuomboleza wala wasikate pembe za ndevu zao wala kujichanja chale mwilini.

6. Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao wala wasilikufuru jina la Mungu wao. Maana wao ndio wanaotolea zile sadaka anazopewa Mwenyezi-Mungu kwa moto yaani chakula cha Mungu. Basi, ni lazima wawe watakatifu.

7. Kwa kuwa kuhani amewekwa wakfu kwa Mungu wake, kamwe asioe kahaba, wala mwanamke asiye bikira wala aliyepewa talaka.

Kusoma sura kamili Walawi 21