Agano la Kale

Agano Jipya

Walawi 18:20-30 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Kamwe usilale na mke wa jirani yako na hivyo kujitia mwenyewe najisi naye.

21. “Kamwe usimtoe mtoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utalikufuru jina langu mimi Mungu wako. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.

22. “Kamwe usilale na mwanamume mwenzio kana kwamba ni mwanamke. Hilo ni chukizo.

23. Kamwe usilale na mnyama ili usijitie najisi; mwanamume au mwanamke yeyote kamwe asifanye hivyo; kufanya hivyo ni upotovu.

24. “Msijitie najisi kwa kufanya mambo hayo kwani kwa sababu ya mambo hayo nayafukuza mataifa yaliyo mbele yenu kwa vile wao hufanya hayo na kujitia najisi.

25. Nchi yao ilitiwa unajisi nami nikaiadhibu, nayo ikawakataa wakazi wake.

26. Lakini nyinyi na wageni wanaokaa kati yenu ni lazima kuyashika masharti na maagizo yangu na wala msifanye machukizo hayo.

27. Machukizo hayo waliyafanya watu waliokaa katika nchi ya Kanaani kabla yenu, nao wakaitia nchi unajisi.

28. Basi, nyinyi msifanye mambo hayo, la sivyo nchi hiyo itawatapika kama ilivyolitapika taifa lililokuwa kabla yenu.

29. Watu wote watakaofanya mambo hayo ya kuchukiza ni lazima watengwe mbali na watu wao.

30. Kwa hiyo shikeni kikamilifu yote ninayowaagiza; msifuate mazoea yoyote ya kuchukiza yaliyofanywa na wale walioishi nchini kabla yenu, msije mkajitia unajisi kwayo. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.”

Kusoma sura kamili Walawi 18