Agano la Kale

Agano Jipya

Walawi 13:8-11 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Kuhani atamwangalia tena, na kama ule upele umeenea kwenye ngozi, basi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi; huo ni ukoma.

9. “Kama mtu ameshikwa na ukoma, ataletwa kwa kuhani.

10. Kuhani atamwangalia na kama kuna uvimbe mweupe ambao umezifanya nywele zake ziwe nyeupe na uvimbe huo umegeuka kuwa kidonda kibichi,

11. huo ni ukoma wa muda mrefu. Kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hakuna haja ya kumweka mtu huyo kwa uchunguzi kwani yu najisi tayari.

Kusoma sura kamili Walawi 13