Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 8:9-12 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Gideoni akawaambia, “Nitakaporudi kwa amani nitaubomoa mnara huu.”

10. Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao la watu 15,000 ambao ndio tu waliobaki kutoka jeshi la mashariki, maana wenzao 120,000 waliuawa.

11. Gideoni akafuata njia ya magharibi iliyo mashariki mwa Noba na Yogbeha, akalishambulia jeshi hilo ambalo halikuwa tayari.

12. Wafalme wa Midiani, Zeba na Salmuna walitoroka wakakimbia, lakini Gideoni aliwafuatia, akawakamata na kulitia jeshi lote hofu kubwa.

Kusoma sura kamili Waamuzi 8