Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 5:4-7 Biblia Habari Njema (BHN)

4. “Ee Mwenyezi-Mungu, ulipotoka huko Seiri,ulipoteremka mlimani Edomu,nchi ilitetemeka,mbingu zilidondosha maji,naam, mawingu yakaiangusha mvua.

5. Milima ilitikisika mbele yako Mwenyezi-Mungu,naam, mlima Sinai mbele yako Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.

6. “Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi,katika wakati wa Yaeli,misafara ilikoma kupita nchini,wasafiri walipitia vichochoroni.

7. Wakulima walikoma kuwako,walikoma kuwako katika Israeli,mpaka nilipotokea mimi Debora,mimi niliye kama mama wa Israeli.

Kusoma sura kamili Waamuzi 5