Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 5:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. “Sikilizeni, enyi wafalme!Tegeni sikio, enyi wakuu!Nitamwimbia Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.

4. “Ee Mwenyezi-Mungu, ulipotoka huko Seiri,ulipoteremka mlimani Edomu,nchi ilitetemeka,mbingu zilidondosha maji,naam, mawingu yakaiangusha mvua.

5. Milima ilitikisika mbele yako Mwenyezi-Mungu,naam, mlima Sinai mbele yako Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.

6. “Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi,katika wakati wa Yaeli,misafara ilikoma kupita nchini,wasafiri walipitia vichochoroni.

Kusoma sura kamili Waamuzi 5