1. Siku hiyo, Debora na Baraki, mwana wa Abinoamu, wakaimba wimbo huu:
2. “Viongozi walijitokeza kuongoza Israeli,watu walijitolea kwa hiari yao.Mshukuruni Mwenyezi-Mungu!
3. “Sikilizeni, enyi wafalme!Tegeni sikio, enyi wakuu!Nitamwimbia Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.
4. “Ee Mwenyezi-Mungu, ulipotoka huko Seiri,ulipoteremka mlimani Edomu,nchi ilitetemeka,mbingu zilidondosha maji,naam, mawingu yakaiangusha mvua.