Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 13:22-25 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Basi, Manoa akamwambia mkewe, “Hakika tutakufa, maana tumemwona Mungu.”

23. Lakini mkewe akamjibu, “Kama Mwenyezi-Mungu angetaka kutuua hangepokea sadaka yetu ya kuteketezwa na ya nafaka; wala hangetuonesha mambo hayo wala kutuambia maagizo.”

24. Kisha mkewe Manoa akajifungua mtoto wa kiume, naye Manoa akampa jina Samsoni. Mtoto huyo akakua naye Mwenyezi-Mungu akambariki.

25. Roho ya Mwenyezi-Mungu ikaanza kumsukuma akiwa huko Mahane-dani, kati ya Sora na Eshtaoli.

Kusoma sura kamili Waamuzi 13