Agano la Kale

Agano Jipya

Sefania 3:9-13 Biblia Habari Njema (BHN)

9. “Wakati huo nitaibadili lugha ya watu,nitawawezesha kusema lugha adiliili waniite mimi Mwenyezi-Mungu,na kuniabudu kwa moyo mmoja.

10. Kutoka ng'ambo ya mito ya Kushiwatu wangu wanaoniomba ambao wametawanyika,wataniletea sadaka yangu.

11. “Siku hiyo, haitakulazimu kuona aibu,kutokana na matendo yako ya kuniasi,maana nitawaondoa miongoni mwakowale wanaojigamba na kujitukuzanawe hutakuwa na kiburi tena katika mlima wangu mtakatifu.

12. Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevuambao watakimbilia usalama kwangu mimi Mwenyezi-Mungu.

13. Waisraeli watakaobaki,hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo;wala kwao hatapatikana mdanganyifu yeyote.Watapata malisho na kulalawala hakuna mtu atakayewatisha.”

Kusoma sura kamili Sefania 3