Agano la Kale

Agano Jipya

Sefania 3:8-10 Biblia Habari Njema (BHN)

8. “Kwa hiyo ningojeni mimi Mwenyezi-Mungu,ngoja siku nitakapoinuka kutoa mashtaka.Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme,kuyamwagia ghadhabu yangu,kadhalika na ukali wa hasira yangu.Dunia yote itateketezwakwa moto wa ghadhabu yangu.

9. “Wakati huo nitaibadili lugha ya watu,nitawawezesha kusema lugha adiliili waniite mimi Mwenyezi-Mungu,na kuniabudu kwa moyo mmoja.

10. Kutoka ng'ambo ya mito ya Kushiwatu wangu wanaoniomba ambao wametawanyika,wataniletea sadaka yangu.

Kusoma sura kamili Sefania 3