Agano la Kale

Agano Jipya

Sefania 3:12-16 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevuambao watakimbilia usalama kwangu mimi Mwenyezi-Mungu.

13. Waisraeli watakaobaki,hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo;wala kwao hatapatikana mdanganyifu yeyote.Watapata malisho na kulalawala hakuna mtu atakayewatisha.”

14. Imba kwa sauti, ewe Siyoni,paza sauti ee Israeli.Furahi na kushangilia kwa moyo wote, ewe Yerusalemu!

15. Mwenyezi-Mungu amekuondolea hukumu iliyokukabili,amewageuzia mbali adui zako.Mwenyezi-Mungu, mfalme wa Israeli yuko pamoja nawehutaogopa tena maafa.

16. Siku hiyo, mji wa Yerusalemu utaambiwa:“Usiogope, ee Siyoni,usilegee mikono.

Kusoma sura kamili Sefania 3