Agano la Kale

Agano Jipya

Sefania 3:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ole wake mji wa Yerusalemu,mji mchafu, najisi na mdhalimu.

2. Hausikilizi onyo lolote,wala haukubali kukosolewa.Haukumtegemea Mwenyezi-Mungu kamwe,wala kumkaribia Mungu wake.

3. Viongozi wake ni simba wangurumao,mahakimu wake ni mbwamwitu wenye njaa jioniwasioacha chochote mpaka asubuhi.

4. Manabii wake ni watu wasiojali na wadanganyifu.Makuhani wake wamevitia unajisi vitu vitakatifuna kuihalifu sheria kwa nguvu.

Kusoma sura kamili Sefania 3