Agano la Kale

Agano Jipya

Sefania 1:9-16 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Siku hiyo nitawaadhibu wote:Wanaoruka kizingiti cha nyumba kama wapagani,wanaojaza nyumba ya bwana wao vitu vya dhuluma na wizi.

10. “Siku hiyo, nasema mimi Mwenyezi-Mungu,Kutasikika kilio kutoka Lango la Samaki,maombolezo kutoka Mtaa wa Pili,na mlio mkubwa kutoka milimani.

11. Lieni enyi wakazi wa Makteshi!Wafanyabiashara wote wameangamia,wote wapimao fedha wamefutiliwa mbali.

12. Wakati huo nitaupekua mji wa Yerusalemu kwa taa,nitawaadhibu wanaoishi wametulia kama machicha ya divai,wote ambao husema mioyoni mwao:‘Mwenyezi-Mungu hatafanya kitu: Chema au kibaya.’

13. Utajiri wao utanyakuliwa,na nyumba zao zitaachwa tupu!Watajijengea nyumba, lakini hawataishi humo.Watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.”

14. Ile siku kubwa ya Mwenyezi-Mungu imekaribia,iko karibu na inakuja mbio.Mlio wa siku ya Mwenyezi-Mungu ni wa uchungu;hapo, shujaa atalia kwa sauti.

15. Siku hiyo itakuwa siku ya ghadhabu,ni siku ya dhiki na uchungu,siku ya giza na huzuni;siku ya uharibifu na maangamizi,siku ya mawingu na giza nene.

16. Siku hiyo ni ya mlio wa tarumbeta ya vita,dhidi ya miji yenye ngome na kuta ndefu.

Kusoma sura kamili Sefania 1