Agano la Kale

Agano Jipya

Sefania 1:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amenia, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa mfalme Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda:

2. Mwenyezi-Mungu asema:“Nitavifagilia mbali viumbe vyote duniani:

3. Wanadamu, wanyama, ndege wa anganina samaki wa baharini;vyote nitaviangamiza.Waovu nitawaangamiza kabisa;wanadamu nitawafagilia mbali duniani.

4. Nitaunyosha mkono wangu dhidi ya nchi ya Yuda,kadhalika na wakazi wote wa mji wa Yerusalemu.Nitaangamiza mabaki yote ya Baali kutoka nchi hii,na hakuna atakayetambua jina lao.

5. Nitawaangamiza wote wanaosujudu juu ya paa,wakiabudu jeshi la mbinguni.Nitawaangamiza wale wanaoniabuduna kuapa kwa jina langu,hali wanaapa pia kwa jina la mungu Milkomu.

6. Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Mwenyezi-Munguwote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.”

7. Nyamazeni mbele ya Bwana Mwenyezi-Mungu,kwani siku ya Mwenyezi-Mungu iko karibu.Mwenyezi-Mungu ameandaa tambiko,nao aliowaalika amewateua.

8. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Katika siku ile ya karamu yangu,nitawaadhibu viongozi wa watu hao,kadhalika na wana wa mfalmepamoja na wote wanaoiga desturi za kigeni.

9. Siku hiyo nitawaadhibu wote:Wanaoruka kizingiti cha nyumba kama wapagani,wanaojaza nyumba ya bwana wao vitu vya dhuluma na wizi.

Kusoma sura kamili Sefania 1