Agano la Kale

Agano Jipya

Ruthu 1:18-21 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Naomi alipoona kuwa Ruthu ameamua kwenda pamoja naye, aliacha kumshawishi.

19. Ndipo wote wawili wakaendelea na safari hadi Bethlehemu. Walipofika huko, watu wote walishangaa, hata wanawake wakaulizana, “Je, huyu ni Naomi?”

20. Naomi akasema, “Msiniite tena Naomi niiteni Mara, kwa maana Mungu mwenye nguvu ameyafanya maisha yangu yawe machungu mno.

21. Nilipoondoka hapa, nilikuwa na vitu vingi, lakini sasa Mwenyezi-Mungu amenirudisha mikono mitupu. Mbona mwaniita Naomi na hali Mwenyezi-Mungu ameniadhibu, naye Mungu Mwenye Nguvu amenitesa.”

Kusoma sura kamili Ruthu 1