Agano la Kale

Agano Jipya

Ruthu 1:17-22 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Pale utakapofia hapo nitakufa nami,na papo hapo nitazikwa;Mwenyezi-Mungu anipe adhabu kali kama nikitenganishwa naweisipokuwa tu kwa kifo.”

18. Naomi alipoona kuwa Ruthu ameamua kwenda pamoja naye, aliacha kumshawishi.

19. Ndipo wote wawili wakaendelea na safari hadi Bethlehemu. Walipofika huko, watu wote walishangaa, hata wanawake wakaulizana, “Je, huyu ni Naomi?”

20. Naomi akasema, “Msiniite tena Naomi niiteni Mara, kwa maana Mungu mwenye nguvu ameyafanya maisha yangu yawe machungu mno.

21. Nilipoondoka hapa, nilikuwa na vitu vingi, lakini sasa Mwenyezi-Mungu amenirudisha mikono mitupu. Mbona mwaniita Naomi na hali Mwenyezi-Mungu ameniadhibu, naye Mungu Mwenye Nguvu amenitesa.”

22. Hivyo ndivyo Naomi pamoja na Ruthu Mmoabu, mkwewe, walivyorejea kutoka Moabu, na kuwasili Bethlehemu wakati uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.

Kusoma sura kamili Ruthu 1