9. Nao Bakbukia na Uno rafiki zao, walisimama ibadani mkabala nao.
10. Yeshua alimzaa Yoyakimu, Yoyakimu alimzaa Eliashibu, Eliashibu alimzaa Yoyada,
11. Yoyada alimzaa Yonathani na Yonathani akamzaa Yadua.
12. Yoyakimu alipokuwa kuhani mkuu, makuhani wafuatao walikuwa wakuu wa koo zao: Wa Seraya, Meraya; wa Yeremia, Hanania;
13. wa Ezra, Mehulamu; wa Amaria, Yehohanani;
14. wa Maluki, Yonathani; wa Shebania, Yosefu;
15. wa Harimu, Adna; wa Merayothi, Helkai;
16. wa Ido, Zekaria; wa Ginethoni, Meshulamu;
17. wa Abiya, Zikri; ukoo wa Miniamini; wa Moadia, Piltai;
18. wa Bilga, Shamua; wa Shemaya, Yehonathani;
19. wa Yoaribu, Matenai; wa Yedaya, Uzi;
20. wa Salai, Kalai; wa Amoki, Eberi;