5. Milima hutetemeka mbele yake,navyo vilima huyeyuka;dunia hutetemeka mbele yake,ulimwengu na vyote vilivyomo.
6. Nani awezaye kuikabili ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu?Nani awezaye kustahimili ukali wa hasira yake?Yeye huimwaga hasira yake iwakayo kama moto,hata miamba huipasua vipandevipande.
7. Mwenyezi-Mungu ni mwema,yeye ni ngome ya usalama wakati wa taabu.Yeye huwalinda wote wanaokimbilia usalama kwake.
8. Adui wakiivamia nchi kama mafuriko, yeye huwaangamiza;huwafuatia na kuwafukuza mpaka gizani.
9. Mbona mnafanya mipango dhidi ya Mwenyezi-Mungu?Yeye atawakomesha na kuwaangamiza,wala mpinzani wake hataweza kuinuka tena.
10. Watateketezwa kama kichaka cha miiba,kama vile nyasi zilizokauka.
11. Kwako kumetoka aliyepanga maovu dhidi ya Mwenyezi-Mungualiyefanya njama za ulaghai.
12. Mwenyezi-Mungu awaambia hivi watu wake:“Ingawa Waashuru ni wengi na wenye nguvu,wao wataangushwa na kuangamizwa.Ingawa nimewatesa nyinyi watu wangu,sitawateseni tena zaidi.
13. Sasa nitaivunja nira ya Ashuru shingoni mwenu,na minyororo waliyowafungia nitaikatakata.”
14. Mwenyezi-Mungu ameamuru hivi kuhusu Ninewi:“Hutapata wazawa kulidumisha jina lako.Sanamu zako za kuchonga na za kusubu,nitazivunjavunja nyumbani mwa miungu yako.Mimi nitakuchimbia kaburi lako,maana wewe hufai kitu chochote.”
15. Enyi watu wa Yuda tazameni:Anakuja kutoka mlimani mtu anayeleta habari njema,mjumbe ambaye anatangaza amani.Adhimisheni sikukuu zenu, enyi watu wa Yuda,timizeni nadhiri zenu,maana waovu hawatawavamia tena,kwani wameangamizwa kabisa.