26. Tena akasema,“Shemu na abarikiwe na Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu!Kanaani na awe mtumwa wake.
27. Mungu na amkuze Yafethi,aishi katika hema za Shemu;Kanaani na awe mtumwa wake.”
28. Baada ya gharika, Noa aliishi miaka 350,
29. kisha akafariki akiwa na umri wa miaka 950.