Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 9:15-21 Biblia Habari Njema (BHN)

15. nitalikumbuka agano langu nanyi na viumbe vyote hai. Kamwe maji hayatageuka kuwa gharika ya kuviangamiza viumbe vyote hai.

16. Huo upinde utakapotokea mawinguni, nitauona na kulikumbuka agano hilo la milele kati yangu na viumbe vyote hai duniani.”

17. Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya agano ambalo nimefanya na viumbe vyote hai duniani.”

18. Watoto wa Noa waliotoka katika safina walikuwa Shemu, Hamu na Yafethi. Hamu alikuwa baba yake Kanaani.

19. Hao ndio watoto watatu wa Noa, na kutokana nao watu walienea duniani kote.

20. Noa alikuwa mkulima wa kwanza. Alilima shamba la mizabibu,

21. akanywa divai, akalewa, kisha akalala uchi hemani mwake.

Kusoma sura kamili Mwanzo 9