Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 9:13-28 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Naweka upinde wangu mawinguni, nao utakuwa ishara ya agano kati yangu na dunia.

14. Kila nitakapoifunika dunia kwa mawingu, na huo upinde wa mvua utakapoonekana katika mawingu,

15. nitalikumbuka agano langu nanyi na viumbe vyote hai. Kamwe maji hayatageuka kuwa gharika ya kuviangamiza viumbe vyote hai.

16. Huo upinde utakapotokea mawinguni, nitauona na kulikumbuka agano hilo la milele kati yangu na viumbe vyote hai duniani.”

17. Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya agano ambalo nimefanya na viumbe vyote hai duniani.”

18. Watoto wa Noa waliotoka katika safina walikuwa Shemu, Hamu na Yafethi. Hamu alikuwa baba yake Kanaani.

19. Hao ndio watoto watatu wa Noa, na kutokana nao watu walienea duniani kote.

20. Noa alikuwa mkulima wa kwanza. Alilima shamba la mizabibu,

21. akanywa divai, akalewa, kisha akalala uchi hemani mwake.

22. Hamu, baba yake Kanaani, aliuona uchi wa baba yake, akatoka nje na kuwaambia ndugu zake wawili.

23. Lakini Shemu na Yafethi wakatwaa nguo, wakaitanda mabegani mwao, wakaenda kinyumenyume na kuufunika uchi wa baba yao. Waliangalia pembeni, wala hawakuuona uchi wa baba yao.

24. Noa alipolevuka na kujua alivyotendewa na mwanawe mdogo,

25. akasema,“Kanaani na alaaniwe!Atakuwa mtumwa wa watumwa kwa ndugu zake.”

26. Tena akasema,“Shemu na abarikiwe na Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu!Kanaani na awe mtumwa wake.

27. Mungu na amkuze Yafethi,aishi katika hema za Shemu;Kanaani na awe mtumwa wake.”

28. Baada ya gharika, Noa aliishi miaka 350,

Kusoma sura kamili Mwanzo 9