Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 7:20-24 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Yaliongezeka hata kuifunika milima kiasi cha mita saba na nusu.

21. Viumbe wote hai katika nchi wakafa. Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama wa porini, makundi ya viumbe wote katika nchi kavu na wanadamu wote;

22. naam, kila kiumbe hai katika nchi kavu kilikufa.

23. Mungu akaangamiza kila kiumbe kilichokuwa hai duniani: Binadamu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Vyote viliangamizwa duniani. Noa tu ndiye aliyesalimika na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.

24. Maji hayo yalidumu katika nchi siku 150.

Kusoma sura kamili Mwanzo 7