Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 5:3-18 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Adamu alipokuwa na umri wa miaka 130, alipata mtoto aliyefanana naye, na mwenye sura kama yake; akamwita Sethi.

4. Baada ya kumzaa Sethi, Adamu aliishi miaka 800, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

5. Adamu alifariki akiwa na umri wa miaka 930.

6. Sethi alipokuwa na umri wa miaka 105, alimzaa Enoshi.

7. Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

8. Sethi alifariki akiwa na umri wa miaka 912.

9. Enoshi alipokuwa na umri wa miaka 90, alimzaa Kenani.

10. Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

11. Enoshi alifariki akiwa na umri wa miaka 905.

12. Kenani alipokuwa na umri wa miaka 70, alimzaa Mahalaleli.

13. Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

14. Kenani alifariki akiwa na umri wa miaka 910.

15. Mahalaleli alipokuwa na umri wa miaka 65, alimzaa Yaredi.

16. Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

17. Mahalaleli alifariki akiwa na umri wa miaka 895.

18. Yaredi alipokuwa na umri wa miaka 162, alimzaa Henoki.

Kusoma sura kamili Mwanzo 5