Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 5:27-32 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Methusela alifariki akiwa na umri wa miaka 969.

28. Wakati Lameki alipokuwa na umri wa miaka 182, alimzaa mtoto wa kiume.

29. Alimwita mtoto huyo Noa, akisema, “Mtoto huyu ndiye atakayetufariji kutokana na kazi yetu ngumu tunayofanya kwa mikono yetu katika ardhi aliyoilaani Mwenyezi-Mungu.”

30. Baada ya kumzaa Noa, Lameki aliishi miaka 595 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

31. Lameki alifariki akiwa na umri wa miaka 777.

32. Noa alipokuwa na umri wa miaka 500, alimzaa Shemu na Hamu na Yafethi.

Kusoma sura kamili Mwanzo 5