Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 5:20-27 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Yaredi alifariki akiwa na umri wa miaka 962.

21. Henoki alipokuwa na umri wa miaka 65, alimzaa Methusela.

22. Henoki alikuwa mcha Mungu. Baada ya kumzaa Methusela, Henoki aliishi miaka 300 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

23. Henoki aliishi miaka 365.

24. Alikuwa mcha Mungu, akatoweka, kwa maana Mungu alimchukua.

25. Wakati Methusela alipokuwa na umri wa miaka 187, alimzaa Lameki.

26. Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

27. Methusela alifariki akiwa na umri wa miaka 969.

Kusoma sura kamili Mwanzo 5