Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 5:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ifuatayo ni orodha ya wazawa wa Adamu. Wakati Mungu alipomuumba binadamu, alimuumba kwa mfano wake.

2. Aliwaumba mwanamume na mwanamke, kisha akawabariki na kuwapa jina “Binadamu.”

3. Adamu alipokuwa na umri wa miaka 130, alipata mtoto aliyefanana naye, na mwenye sura kama yake; akamwita Sethi.

4. Baada ya kumzaa Sethi, Adamu aliishi miaka 800, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

5. Adamu alifariki akiwa na umri wa miaka 930.

Kusoma sura kamili Mwanzo 5