Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 5:1-11 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ifuatayo ni orodha ya wazawa wa Adamu. Wakati Mungu alipomuumba binadamu, alimuumba kwa mfano wake.

2. Aliwaumba mwanamume na mwanamke, kisha akawabariki na kuwapa jina “Binadamu.”

3. Adamu alipokuwa na umri wa miaka 130, alipata mtoto aliyefanana naye, na mwenye sura kama yake; akamwita Sethi.

4. Baada ya kumzaa Sethi, Adamu aliishi miaka 800, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

5. Adamu alifariki akiwa na umri wa miaka 930.

6. Sethi alipokuwa na umri wa miaka 105, alimzaa Enoshi.

7. Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

8. Sethi alifariki akiwa na umri wa miaka 912.

9. Enoshi alipokuwa na umri wa miaka 90, alimzaa Kenani.

10. Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.

11. Enoshi alifariki akiwa na umri wa miaka 905.

Kusoma sura kamili Mwanzo 5